Proverbs 26

1 aKama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno,
ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.

2 bKama shomoro apigapigavyo mabawa yake
au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi,
ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.

3 cMjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,
nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!

4 dUsimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,
ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.

5 eMjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,
ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.

6 fKama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara,
ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.

7 gKama miguu ya kiwete inavyoningʼinia
ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.

8 hKama kufunga jiwe kwenye kombeo,
ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.

9 iKama mwiba kwenye mkono wa mlevi
ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.

10Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo,
ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.

11 jKama mbwa ayarudiavyo matapiko yake,
ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.

12 kJe, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima
machoni pake mwenyewe?
Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.

13 lMvivu husema, “Yuko simba barabarani,
simba mkali anazunguka mitaa!”

14 mKama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake,
ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.

15 nMtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani,
naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.

16Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe,
kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.

17Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio,
ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.

18Kama mtu mwendawazimu
atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 ondivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema,
“Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”

20 pBila kuni moto huzimika;
pasipo uchongezi ugomvi humalizika.

21 qKama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto,
ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.

22 rManeno ya mchongezi ni kama chakula kitamu;
huingia sehemu za ndani sana za mtu.

23 sKama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo
ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.

24 tMtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake,
lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 uIngawa maneno yake huvutia, usimwamini,
kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu,
lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.

27 vKama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake,
kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.

28 wUlimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza,
nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Copyright information for SwhNEN